Proverbs 25:2-7


2 aNi Utukufu wa Mungu kuficha jambo,
bali ni utukufu wa wafalme kuchunguza jambo.


3 Kama mbingu zilivyo juu na nchi ilivyo chini,
ndivyo ambavyo mioyo ya wafalme haichunguziki.


4 bOndoa takataka kwenye madini ya fedha,
nako ndani yake kutatokea chombo
cha mfua fedha.

5 cOndoa waovu mbele ya mfalme,
nacho kiti chake cha enzi
kitaimarishwa kwa njia ya haki.


6 Usijikweze mwenyewe mbele ya mfalme,
wala usidai nafasi miongoni mwa watu wakuu;

7 dni afadhali yeye akuambie, “Njoo huku juu,”
kuliko yeye kukuaibisha mbele ya mkuu.

Kile ulichokiona kwa macho yako
Copyright information for SwhKC